Kutunza
Mazingira Katika Pwani ya Magharibi ya Senegal
Hifadhi
ya Asili ya Ker Cupaam iko katika eneo la “Petite Cote” la Senegal,
kilomita 45 kusini mwa Dakar kwenye pwani ya Atlantiki. Sehemu hii
ya msitu wa asili wenye ukubwa wa takribani hekta 100 ilitengwa
kwa amri ya serikali mwanzoni mwa miaka ya 1980 ili kulinda makazi
ya majira ya baridi ya ndege aina ya “blue grackle” na “rock grackle”
ambao walikuwa hatarini kutoweka, na kuhifadhi njia wanayotumia
ndege wengi wanaohamia kwenye pwani ya Atlantiki ya Afrika Magharibi.
Majabali yanayopakana na ufuko kwenye eneo hili la pwani yanafaa
sana kama mahali pa kuzalia na malisho kwa aina nyingi za ndege. Kukabili
changamoto
Ingawa
katiba ya hifadhi ya asili mwanzoni mwa miaka 1980 ilisaidia kusimamisha
uharibifu zaidi wa mazingira, mimea mingi katika eneo ilikuwa imeharibiwa
mno kiasi kwamba juhudi kubwa zilihitajika kurejesha ustawi wa zamani
na kuvutia shughuli za kitalii ambazo zingewaletea faida wenyeji
wa eneo hili. Hilo ndilo hitimisho lililofikiwa na kikundi cha wanawake
kutoka kijiji cha Popenguine, ambao mwaka 1988 walianzisha Umoja
wa Wanawake wa Popenguine wa Kuhifadhi Mazingira (Regroupment des
Femmes de Popenguine pour la Protection de la Nature – au “RFPPN”).
Kikundi kilijumuisha awali wanawake 119 na mwanamume mmoja, ambaye
alitokea kuhudhuria mkutano wa uanzilishi wa Umoja huo. Walimchagua
mungu Mame Cumba Cupaam,
“roho wa wavuvi wa pwani”, kuwa matroni (mlezi) wao. Katika
kipindi cha miaka minane iliyofuata, umoja wa “RFPPN” ulitumia kwanza rasilimali zake na kisha za nyongeza kutoka kwa
mashirika ya wafadhili yaliyounga mkono usimamizi wa aina hii wa
maliasili ili kurejesha upya ustawi wa awali wa mimea ya hifadhi
na eneo la karibu na hifadhi. Hatua zilizotekelezwa na Umoja huu
ni pamoja na utengenezaji wa vizuizi vya moto kuzunguka hifadhi
yote, upandaji upya wa mimea ya asili kwa eneo hili kwa kutumia
miche ya kitalu kilichoanzishwa sawia na wanawake, na kuandaa warsha
ambapo vijana wa kujitolea kutoka vijiji na miji jirani waliletwa
kujifunza hifadhi ya maliasili na kufanya kazi kwa vitendo iliyohitajika. Kwenda
kwenye kiini cha jambo
Zaidi
ya hayo, Umoja wa “RFPPN” ulishughulikia mara moja tishio kuu la
kurejesha na kuhifadhi ustawi wa mazingira: ukataji miti ovyo kwa
ajili ya kuni uliokuwa ukifanywa na wanavijiji wa eneo hili. Wanawake
waliazimia kutafuta nishati mbadala na kuzifanya jumuiya zao ziwe
na nishati ya kutosha ya kupikia. ·
Kwanza,
walianzisha mtandao wa ushirika wa kusambaza kuni, mkaa na gesi
ili kudhibiti matumizi na kuwasaidia wanachama wao kupata mahitaji
ya kaya zao. ·
Pili,
walianzisha kitalu cha miche ya miti cha kijiji na msitu wa jumuiya
ili viwe vyanzo vya awali vya nishati ya kupikia. ·
Mwisho,
walianzisha utaratibu wa kukusanya takataka za kila kaya na kuzirundika
ili kuzuia madhara ya uchafu kwa afya za wananchi yanayotokana na
utupaji ovyo wa takataka na pia kuzalisha mbolea kwa ajili ya kitalu
cha miche ya miti. Kwa
kufanya hivi, wanawake sio tu walifaulu kurejesha bioanuwai na mimea
ya asili ya eneo hili, bali pia juhudi zao ziliwezesha kurejesha
eneoni aina mbalimbali za viumbe ambao walikuwa hawaonekani kwa
miaka mingi:aina nyingi za ndege; nungunungu, nguchiro, tumbili,
mbweha, ngawa, na hata paa. Kujenga
mtandao Juhudi
zao hatimaye zilifikia kiwango ambapo ustawishaji upya wa mazingira
ya eneo lao usingekuwa na mafanikio bila ushiriki mpana wa vijiji
vya jirani. Kwa kweli programu na mfano wa Umoja wa “RFPPN” viliongeza
hamasa miongoni mwa watu wa jumuiya za jirani. Badala ya kuupanua
Umoja wa “RFPPN”, wanachama wa Umoja wa Popenguine waliamua kuwatia
moyo wanawake wa vijiji vya jirani kuanzisha vyama vyao na vitalu
vyao vya miche, na pia taratibu na mitandao yao ya kugawa nishati
ya kupikia. Hatimaye jumuiya nane zilishirikishwa na Umoja wa Popenguine
chini ya kamati ya pamoja ya uratibu, na hivyo kufanya wanachama
wa programu kuongezeka kutoka wale 119 wa awali hadi kufikia zaidi
ya wanachama 1500. Maelfu ya miche mipya sasa huzalishwa kila mwaka
na mtandao huu wa vyama. Wakati
huohuo, vikundi vya wanawake viliongeza nyanja nyingine mpya kwenye
programu yao. Nyanja tatu zaidi zinazojalizana zimeongezeka kutokana
na msaada wa Jumuiya ya Uchumi ya Ulaya. ·
Mikopo
na huduma za benki: Ili kupunguza umasikini uliokithiri uliopelekea
kwenye uharibifu wa mazingira, vyama vilianzisha benki za nafaka,
huduma za mikopo na ukulima mdogomdogo wa umwagiliaji wa mboga za
majani katika kila kijiji. Kilimo cha mboga kilihamasisha ukusanyaji
wa takataka ili kutengeneza mbolea iliyohitajika bustanini. ·
Miundombinu
ya utalii na mafunzo: kutokana na watu wa Senegal nzima na hata
wa nchi za nje kuvutiwa sana na majaribio ya Popenguine, wanawake
waliamua kujenga miundombinu rahisi kwa ajili ya kuwahifadhi wageni
wao waliowatembelea kujifunza ujuzi toka kwao. Hii ilifuatiwa na
kuanzisha Kituo cha Mafunzo ya Usimamizi wa Ikolojia” (Centre for
Training in Ecological Management). Sasa walipata vikundi vya wageni
kutoka nchi kadhaa za kigeni ambao walivutiwa sana na mfano huu
uliofaulu wa maendeleo ya ikolojia. ·
Ajira
ya vijana: ili kuzuia uhamaji wa vijana wa vijana wanaohitimu shule
na kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana wa eneo zima,
vyama viliwekea mkazo maalum kuwafundisha vijana shughuli mbalimbali
za kiuchumi zilizokuwa zimeanzishwa katika hifadhi hii mpya. Watu
wa kujitolea kutoka vijiji na miji ya jirani wamepatiwa kazi ya
kurejesha ustawi wa hifadhi na kujifunza misingi ya usimamizi mzuri
wa ikolojia. Baadhi ya watu hawa wamepata ajira za kudumu. Ajira
nyingi hushughulikiwa na vilabu vya vijana wa Kisenegal vinavyoshirikiana
na Mfuko wa Nicolas Hulot, NGO ya Kifaransa inayoshughulikia hifadhi
ya mazingira duniani kote. Hifadhi
na eneo linalolindwa sasa lina ukubwa wa zaidi ya maili 50 za mraba
na hutoa fursa zaidi za maisha kwa jumuiya zinazopakana na eneo
hili. Uwepo wa pamoja kati ya hifadhi ya kitaifa ya Kiafrika na
wananchi majirani ni ishara ya mtindo mpya na wa matumaini wa kuhifadhi
mazingira. Umoja wa “RFPPN” umeipatia Senegal na vikundi vinginevyo
katika nchi za Kiafrika mfano wa usimamizi wa ikolojia uliobuniwa
na wenyeji, na unaotoa faida katika muda mfupi kwa mazingira na
watu wanaoishi katika mazingira hayo. *msingi
wa makala hii ni utafiti uliofanywa na watafiti wa Senegal kwa msaada
na ushauri wa kiufundi wa Profesa Peter Easton wa Chuo Kikuu cha
Jimbo la Florida, wakishirikiana na baadhi ya jumuiya za Kiafrika.
Utafiti ulifadhiliwa na Club du Sahel?OECD, CILSS na ADEA. |